Watu wanne
wameuwawa Jumatano asubuhi baada ya ndege ya mzigo kuanguka katika mtaa wa
Utawala mjini Nairobi, na kuharibu majengo mawili kabla ya kuwaka moto.
Walinzi wawili
walokua karibu na majengo hayo ya biashara walijeruhiwa, na kutibiwa hospitali.
Mkuu wa polisi wa County ya Nairobi Benson Kibue amesema ajali hiyo ilitokea
saa kumi alfajiri wakati ndege ya shirika la Skyward kuanguka na kuwaka moto.
Watu wann walokua
ndani ya ndege akiwemo rubani ndio waliuliwa, muda mfupi baada ya ndege hiyo
kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenyatta mjini Nairobi ikiwa
inasafirisha mizigo wa mairungi kuelekea Mogadishu, Somalia.