Wednesday, July 2, 2014

NDEGE YAUWA WATU WANNE NCHINI KENYA







Watu wanne wameuwawa Jumatano asubuhi baada ya ndege ya mzigo kuanguka katika mtaa wa Utawala mjini Nairobi, na kuharibu majengo mawili kabla ya kuwaka moto.

Walinzi wawili walokua karibu na majengo hayo ya biashara walijeruhiwa, na kutibiwa hospitali. Mkuu wa polisi wa County ya Nairobi Benson Kibue amesema ajali hiyo ilitokea saa kumi alfajiri wakati ndege ya shirika la Skyward kuanguka na kuwaka moto.

Watu wann walokua ndani ya ndege akiwemo rubani ndio waliuliwa, muda mfupi baada ya ndege hiyo kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenyatta mjini Nairobi ikiwa inasafirisha mizigo wa mairungi kuelekea Mogadishu, Somalia.