kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon akipeana
mkono na na Mwenyekiti wa timu hiyo Ndugu Said Mohammed
Omog akionyesha jezi aliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Azam FC
Kocha mpya wa klabu ya
Azam FC ameingia nchini, klabu ya Azam inapenda kuufahamisha umma kuwa imeingia
mkataba na kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon kwa kipindi cha miaka
miwili (2) kuanzia jana.
Azam Football Club
inamuona kocha Omog kuwa anakidhi vigezo vya kuendana na dira ya klabu ambayo
ni kukuza na kuwaendeleza wachezaji na kushindana kwa kiwango cha juu kwa lengo
la kuwa mabingwa katika mashindano mabalimbali ambayo timu inashiriki.
Uongozi wa Azam FC
utampatia ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha malengo na mipango thabiti ya
klabu.