Tuesday, August 26, 2014

Tuesday, August 5, 2014

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI JOHN KERRY ASISITIZA MAZUNGUMZO KATI YA ISRAEL NA PALESTINA




Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry amezitaka pande mbili zinazopingana Israel na Palestina kutia maanani usitishwaji wa mapigano huko ukanda wa Gaza na kuketi katika meza ya mazungumzo.

Bwana Kerry ameiambia BBC kuwaa ni lazima kutia maanani katika pande hizo mbili kuridhiana na kusema kwamba Israel inayo haki ya kujitetea na kujilinda dhidi ya mashambulizi ya maroketi yanayorushwa na Palestina na kukilaumu kikundi cha Hamas kwa mashambulizi hayo lakini pia ametambua kile alichokiita uharibifu mkuwa wa mali na maisha ya watu.

Maelfu ya wapalestina waliokua katika ukanda wa Gaza wamerejeshwa makwao chini ya uangalizi wa umoja wa mataifa katika siku ya kwanza ndani ya saa sabini na mbili za makubaliano ya usitishwaji mapigano baina ya vikundi vya askari wa Israel na Palestina.

Israel imetuma ujumbe huko Cairo ,Misri kujadili juu ya Palestina kusitisha mapigano kwa kipindi kirefu.