Thursday, November 29, 2012

KUITWA KWENYE USAILI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS

               SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

  
Kumb. Na. EA.7/96/01/C/67                                                                        30 Novemba, 2012

KUITWA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Mbeya Institute of Science and Technology (MIST), Water Development Management Institute (WDMI) na Tea Research Institute of Tanzania (TRIT) anatarajia kuendesha usaili na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi, waombaji kazi watakaofaulu usaili.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anawatangazia waombaji wa fursa za ajira kwa tangazo lililotolewa tarehe 28/05/2012, 29/06/2012 na 27/07/2012 za Mamlaka za Ajira zilizotajwa hapo juu kuwa wamechaguliwa kufanya usaili.

Wasailiwa wanashauriwa kuzingatia yafuatayo:

  1. UKAGUZI WA VYETI UTAANZA SAA 1:00 HADI 1:30 ASUBUHI SIKU YA MTIHANI WA MCHUJO.

  1. KUJA NA KITAMBULISHO KWA AJILI YA UTAMBUZI MFANO: KITAMBULISHO CHA MKAZI, KUPIGIA KURA, BENKI, KAZI, HATI YA KUSAFIRIA N.K

  1. Kuja na Vyeti Halisi (original certificates) za kuanzia kidato cha nne, sita, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za mwombaji.

  1. “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.

  1. Kila msailiwa aje na picha moja (Passport size).

  1. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi.

  1. Kila msailiwa azingatie tarehe na eneo alilopangiwa kufanyiwa usaili

  1. Kila msailiwa aje na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate)

  1. Wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuomba tena mara nafasi za kazi zitakapotangazwa.

NB: Kwa Maelezo zaidi Tangazo hili linapatikana pia katika tovuti zifuatazo:-

 www.ajira.go.tz,  www.utumishi.go.tz,  www.pmoralg.go.tz, www.trit.or.tz na www.wdmi.go.tz





JENGO JIPYA LA CHUO CHA UHASIBU TANZANIA


Muonekano wa nje wa jengo hilo la Campus ya Dar es Salaam kwa nje

Muonekano wa nje


Mlango mkuu wa kuingilia


Sehemu ya pembeni ya jengo

Ngazi

Kennedy, Hamis, na Kitandu wakishuka mjengoni



Muonekano wa ndani katika jengo jipya


Sehemu ambazo zimetengwa kwa ajili ya sherehe  ndogo na mikutano

Wednesday, November 28, 2012

RAISI KIKWETE AZINDUA UKUMBI MPYA WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

Spika wa Bunge Anne Mkinda akimpokea Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya M. Kikwete wakati alipowasili katika ukumbi huo wa bunge

Spika wa Bunge la Tanzania Mh. Anne Makinda akikaribishwa na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mh. Margret Natongo katika jengo hilo jipya.


Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya M. Kikwete akihutubia Bunge la Afrika Mashariki wakati alipofika kuzindua ukumbi mpya wa Bunge hilo jijini Arusha.


Ukumbi wa Bunge la Afrika Mashariki

Baadhi ya wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na Mh. Raisi Kikwete

Picha na: Othmani Michuzi

Tuesday, November 27, 2012

CECAFA SENIOR CHALLENGE CUP 2012 FIXTURES



Match Day 5
28-11-2012 16:00
Somalia
Sudan
 
28-11-2012 18:00
Tanzania
Burundi

Match Day 6
29-11-2012 16:00
Malawi
Eritrea
 
29-11-2012 18:00
Rwanda
Zanzibar

Match Day 7
30-11-2012 16:00
Kenya
Ethiopia
 
30-11-2012 18:00
South Sudan
Uganda

Match Day 8
01-12-2012 14:00
Sudan
Burundi
 
01-12-2012 14:00
Somalia
Tanzania
 
01-12-2012 16:00
Eritrea
Rwanda
 
01-12-2012 16:00
Malawi
Zanzibar






JB MPIANA KUTUMBUIZA DAR IJUMAA HII

JB Mpiana akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu onyesho lake litakalofanyika ijumaa katika viwanja vya Leaders Club.

Monday, November 26, 2012

MSANII MWIGIZAJ MCHEKESHAJI SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA



Msanii/Muigizaji/Mchekeshaji Hussein Ramadhani Mtioeti (27) maarufu SHARO MILIONEA amefariki dunia katika ajali ya gari jijini Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Prudence Masawe, amethibitisha kutokea kwa ajali na kusema kuwa marehemu amefikwa na umauti baada ya gari lake aina ya Toyota Haria lenye namba za usajili T478 BVR kuacha njia na kupinduka.

Hili ni pigo jingine kwa Tasnia ya Filamu nchini Tanzania, hasa ukizingatia kuwa juma lililopita alifariki msanii Mlopelo na wakati Sharo Milionea anafariki tayari tasnia hiyo ya bongo Move ipo katika Msiba mwingine mzito wa Mcheza Filamu John Steven anaetarajiwa kuzikwa kesho.
Kamanda Massawe amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa mbili usiku wa Novemba 26, 2012 katika kijiji cha Maguzoni Soga Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.

Akisimulia zaidi RPC Massawe anasema kuwa marehemu alikuwa akiendesha gari hilo na alikuwa peke yake bila abiria mwingine na ajali kumfika akiwa katika kijiji hicho kilichopo kati ya segera na Muheza.

“Marehemu ndie alikuwa akiendesha gari lile, na lililopopinduika yeye alirushwa nje lkupitia kiooo cha mbele na umauti kumfika hapo hapo” alisema Kamanda Massawe.

Aidha Kamanda Massawe amesema msanii huyo alikuwa akitokea jijini Dar es Salaam na alikuwa akienda nyumbani kwao Muheza.

Inakumbukwa kuwa Msanii huyo aliyejizolea umaarufu mkubwa kwa staili yake ya utembeaji na uongeaji alipata al;inusurika katika ajali nyinge mapema mwaka huu baada ya basi alilokuwa akisafiria la Taqwa kutoka nchi jirani ya Burundi kupata ajali Mikese mjini Morogoro Januari 5 mwaka huu akirejea Dar es Salaam.

Habari na Father Kidevu

Sunday, November 25, 2012

AJALI JIJINI MBEYA

Ajali hii imetokea maeneo ya barabara ya Mbalizi kuelekea Mabatini baada ya gari hilo mali ya Kampuni ya Vodacom kuvamia nguzo ya taa za barabarani.


Saturday, November 24, 2012

MKUU WA MAJESHI DRC AFUTWA KAZI


Mkuu wa majeshi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amesimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea kufuatia madai kuwa aliwauzia silaha makundi ya waasi yanaopambana na serikali ya nchi hiyo.
Ripoti moja ya Umoja wa Mataifa, imemtuhumu, Generali Gabriel Amisi kwa kuendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa wawindaji haramu na makundi ya waasi, likiwemo kundi la Mai Mai Raia Mutomboki.
Msemaji wa serikali ya nchi hiyo amesema, maafisa kadhaa wa jeshi pia wanachunguzwa.
Serikali ya Rais Kabila imemfuta kazi mkuu huyo wa majeshi, siku chache baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Goma Mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi hao mpia wameutekja mji wa Sake, lakini msemaji wa serikali Lambert Mende, amesema wanajeshi wa serikali wamefanikiwa kuumboa tena mji huo mdogo.
Waasi hao ambao wanaaminika kuungwa mkono na serikali za Rwanda na Uganda, wametishia kuendeleza mapigano hayo hadi mji mkuu wa Kinshasa, ikiwa rais Joseph Kabila hatabuli kuanzisha mazungumzo ya amani.

Thursday, November 22, 2012

MLOPELO AMEFARIKA DUNIA

Taarifa zilizopatikana jana jioni zinaeleza kuwa aliyewahi kuwa muigizaji katika kikundi cha Kaole,(pichani enzi za uhai wake) ,aliyekuwa akitambulika kwa jina la Mlopelo amefarika dunia mapema jana katika hospitali ya Temeke,jijini Dar,kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa marehemu wamesema Mlopelo amefarika mchana wa jana kwenye hospitali ya Temeke, na kwamba shughuli zote za Msiba zipo nyumbani kwao Temeke Wailess mtaa wa Boko

Wednesday, November 21, 2012

DI MATTEO AFUTWA KAZI


Roberto Di Matteo amefutwa kazi na klabu ya Chelsea, baada ya kuwa meneja kwa kipindi cha miezi minane.
Di Matteo aliiwezesha Chelsea kuwa mshindi wa klabu bingwa barani Ulaya, na vile vile kupata Kombe la FA msimu uliopita, na mwezi Juni, alitia saini mkataba wa miaka miwli.
Lakini kufuatia Chelsea kuzabwa magoli 3-0 na Juventus usiku wa Jumanne, inaelekea timu hiyo itakuwa na kibarua kigumu sana cha kufanikiwa kuendelea katika michuano ya klabu bingwa, na kwa hiyo wasimamizi wa klabu wameonelea ni vyema kumtimua kutoka Stamford Bridge.
Kulingana na taarifa katika mtandao wa Chelsea, "klabu kitatoa taarifa kamili hivi karibuni kuhusiana na meneja wa timu".
Roman Abramovich, tajiri anayemiliki klabu ya Chelsea, sasa atakuwa anamtafuta meneja wa tisa, tangu kumiliki klabu mwaka 2003, na kwa muda mrefu, inaaminika amekuwa akizitamani sana huduma za aliyekuwa meneja wa Barcelona ya Uhispania, Pep Guardiola.
Lakini vile vile amewasiliana na aliyekuwa kocha wa Liverpool ya Uingereza, Rafael Benitez, na kuna uwezekano huenda akashikilia hatamu kwa muda mfupi.
Abramovich, raia wa Urusi, tayari alikuwa amewasiliana na Benitez hata kabla ya Chelsea kushindwa nchini Italia.

VACANCY POST - Public Relations Officer II

Public Relations Officer II
Muhimbili National Hospital

Date Listed: Nov 15, 2012
Phone: No Calls Please
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Nov 23, 2012

Position Description:

Reports To: Senior Public Relations Officer       
Duties and Responsibilities:                                        
To prepare daily report on Hospital status for briefing the media       
Assist to prepare Hospital promotional materials for internal and external clients             I              
Assist to develop health education programmes in all types of media to         maintain favorable public and other stakeholders perception)
To ensure proper recording and filing of press cuttings
To monitor the media during press coverage, public speaking on various presentations, news bulletins, radio and TV talks
To take photographs during various Hospital events for internal and external public use
To ensure that all major Hospital events and ceremonies are covered and advertised correctly and widely
To assist in organizing official functions and tours of Hospital's
officials
To assist in organizing and coordination of annual sports Bonanza and MuhimbiliDay
To use media social networks to amplify Hospital activities to wide stakeholder group
To ensure that all issues to be advertised are correctly prepared
To process all Hospital advertisement logistics
To prepare permits for Police to interrogate admitted patients
To accompany journalists with interests to cover news of patients admitted in various wards
To assist in marketing Hospital health services such as health check and other private services (IPPM)
Perform other duties as assigned by your supervisor
Required Qualifications
Holder of a Bachelor's degree in Journalism, Mass Communication, Public Relations or equivalent qualifications from a recognized institution
Strong analytical, communication, strategic planning and interpersonal skills with creativity and highest ethical standards
Good command of both English and Kiswahlli languages
Good working knowledge of computer applications is mandatory.
Application Instructions:

All application letters should be sent by post using the address below and letters delivered by hand shall not be considered.
Applications accompanied with a detailed CV and copies of certificates, testimonials and names of three referees should be addressed to the Executive Director so as to reach her before 23rd November, 2012.
Executive Director
Muhimbili National Hospital, P.O BOX 65000,
Dar es Salaam.