Nahodha wa Cameroon Samwel Eto’o
katika mechi ya kujipima nguvu ambayo The indomitable Lions iliishinda
Macedonia mabao 2-0 nchini Austria.
Etoo alipumziswa huku timu hiyo
ikiendelea kukumbwa na majeraha zaidi kabla ya kombe la dunia.
Mshambulizi huyo wa Chelsea
hakuchezeshwa kutokana na jeraha la goti, huku Cameroon ikimpoteza mshambulizi
mwingine Pierre Webo kutokana na jeraha siku ya Jumatatu punde baada ya
kufunga.
Jean-Eric Maxim Choupo-Moting baadae
akaongeza bao la pili.
Kipa Charles Itandje, mlinzi
Jean-Armel Kana-Biyik na viungo Edgar Salli, Jean II Makoun na Stephane Mbia
wote wanauguza majeraha tofauti.
Cameroon bado wana mechi za kujipima
nguvu dhidi ya Paraguay, Ujerumani na Moldova kabla ya kombe la dunia.