Sunday, December 1, 2013

KOCHA MPYA WA AZAM FC AWASILI NCHINI


kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon akipeana mkono na na Mwenyekiti wa timu hiyo Ndugu Said Mohammed

Omog akionyesha jezi aliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Azam FC


Kocha mpya wa klabu ya Azam FC ameingia nchini, klabu ya Azam inapenda kuufahamisha umma kuwa imeingia mkataba na kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon kwa kipindi cha miaka miwili (2) kuanzia jana.

Azam Football Club inamuona kocha Omog kuwa anakidhi vigezo vya kuendana na dira ya klabu ambayo ni kukuza na kuwaendeleza wachezaji na kushindana kwa kiwango cha juu kwa lengo la kuwa mabingwa katika mashindano mabalimbali ambayo timu inashiriki.

Uongozi wa Azam FC utampatia ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha malengo na mipango thabiti ya klabu.

Tuesday, November 26, 2013

FINANCE AND ADMINISTRATION ASSISTANT – 1 position



REPOA is currently seeking applications from interested individuals for the position of Finance and Administration Assistant.


JOB SUMMARY:

 Reporting to the Senior Accountant, the job holder will provide the Department of Finance and Administration with financial and administrative support.

 Key responsibilities

FINANCE

 a) Process daily payments and ensure that financial transactions are in accordance with REPOA financial rules and regulations

b) Process subsidiary and general ledgers

 c) Provide assistance to ensure proper management of departmental budgets.         

d) Support preparation of final accounts


ADMINISTRATION

 e) Assist in the process of recruitment of staff

f) Assist in updating Human Resource policies and procedures

 g) Provide support in ensuring that Health and Safety Regulations are complied with

 h) Support in coordination of general maintenance and repairs of assets


MINIMUM REQUIREMENTS:

 • A degree in Accountancy/business administration or equivalent qualifications from a recognized Institution.

 • Excellent administrative skills

 • At least one year work experience in accounting department

 • Knowledge of financial systems including PASTEL accounting software

 • Attention to detail and accuracy

 • Excellent communication skills, both written and verbal

 • Ability to work calmly under pressure and keep to deadlines

 • Ability to work independently but also as part of a small team

 • IT literate


MODE OF APPLICATION:

 Qualified applicants are welcome to apply, and should send their typed application letter and detailed CV including three referees to the address below by 3rd December 2013

 
REPOA IS AN EQUAL OPPORTUNITY EMPLOYER.

 Only applicants who meet requirements will be considered for an interview. Those who do not hear from REPOA should consider themselves unsuccessful.

Applications should be addressed to The Executive Director, REPOA

Wednesday, November 13, 2013

ZANZIBAR WAKAMATA MENO YA TEMBO



 
Polisi nchini Tanzania wamekamata vipande elfu moja na ishirini na moja vya meno ya tembo vyenye uzito wa karibu kilo elfu tatu.

Meno hayo ya tembo yamekamatwa katika bandari ya Zanzibar jana na watu wawili wanashikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na meno hayo. Hata hivyo, bado haijafahamika idadi kamili ya tembo waliouawa, kwani baadhi ya meno yamekatwa vipande.

Kwa mujibu wa afisa habari mkuu wa jeshi la polisi Zanzibar, Inspekta Mohammed Mhina, kiasi kilichokamatwa ni kikubwa kuwahi kukamatwa visiwani humo. Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alisema meno hayo yalikuwa yamehifadhiwa katika kontena la futi arobaini yakiwa yamechanganywa katika mifuko iliyohifadhi makombe ya konokono wa baharini, tayari kwa kusafirishwa nje.

Hivi karibuni raia watatu wa China walikamatwa nchini Tanzania kwa kukutwa na meno 706 ya tembo, sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi mbalimbali nchini humo.

Kukamatwa kwa meno haya ya tembo, kumekuja wakati tayari serikali imetangaza kusitisha Operesheni Tokomeza Ujangili, ambayo ililenga kunusuru wanyama walio hatarini kutoweka kutokana na kuuawa katika hifadhi za taifa nchini Tanzania. Wanyama wanaolengwa zaidi na majangili kutokana na meno yao na pembe ni tembo na faru.

Matukio ya kukamatwa kwa meno ya tembo kutoka Afrika Mashariki yamekuwa yakiripotiwa kila mara. Oktoba, 20, 2012, tani nne za meno ya tembo yenye thamani ya dola milioni 3.4 za Kimarekani yalikamatwa Hong Kong, yakidaiwa kusafirishwa kutoka Kenya na Tanzania.

Pia Agosti 16 mwaka huu polisi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, walimkamata raia wa Vietnam akiwa na meno ya tembo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 18 sawa na dola zaidi ya elfu 11, yakisafirishwa kwenda nje.

Friday, November 8, 2013

AZAM FC YAMTIMUA KOCHA


Huku ligi kuu soka Tanzania Bara ikiwa imekamilisha mzunguko wake wa kwanza, timu ya Azam FC ya Dar es Salaam imetangaza kusitisha mkataba na kocha wake mkuu Stewart Hall wa Uingereza kwa kile kilichoelezwa kama makubaliano ya pamoja.
Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa klabu hiyo jijini Dar es Salaam, hii itakuwa ni mara ya pili kwa kocha huyo kuachana na klabu ya Azam na ameafikiana na uongozi wa klabu hiyo baada ya kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ambapo timu ya Azam sasa inashika nafasi ya Pili baada ya kwenda sare ya mabao 3-3 na timu ya Mbeya City ambapo zote sasa zina Pointi 27. Bingwa mtetezi timu ya Yanga inaongoza ligi hiyo kwa sasa ikiwa na pointi 28 baada ya kuinyuka Oljoro JKT mabao 3-0 katika mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo, maaruf kama Vodacom Premier League.
Klabu ya Azam FC inayoinukia kwa ubora wa miundo mbinu huku ikiendeshwa kisasa kwa mipango inayoeleweka kinyume na klabu nyingi nchini Tanzania imekuwa ikifanya vema chini ya mwalimu huyo ambapo msimu uliopita aliiwezesha kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kushika nafasi ya Pili katika Ligi kuu msimu uliopita.
Klabu hiyo inao wachezaji kadhaa wa Kulipwa kutoka nchi za Ivory Coast, Kenya na Uganda. Kuachia ngazi kwa kocha huyo kunaelezwa kuwa kumekuwa kwa mkakati ili kusiathiri mwenendo wa timu hususan wakati ligi ikiendelea na sasa kutaiwezesha Azam FC Kutafuta kocha mwingine hususan wakati huu ambapo ligi imefikia Mapumziko.

Wednesday, October 23, 2013

KAMANDA MSTAAFU WA POLISI JAMES KOMBE AFARIKI DUNIA



Aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha usalama barabarani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) mstaafu James Kombe amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.


Akizungumzia kifo hicho Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Advera Senso alisema, Kombe alifariki Oktoba 22 mwaka huu na taratibu za mazishi zinaendelea.


Aidha Senso alisema Marehemu Kombe alizaliwa mwaka 1950 huko Mwika mkoani Kilimanjaro na alijiunga na Jeshi la Polisi tarehe 15 mwezi machi mwaka 1970 baada ya kuhitimu elimu ya sekondari mwaka 1969 nchini Uganda ambapo alipandishwa vyeo na kupewa madaraka mbalimbali.


Baadhi ya vyeo alivyopitia na miaka ya kupata vyeo hivyo katika mabano ni pamoja na Sagenti wa Polisi (1973) Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (1977), Mkaguzi wa Polisi (1984), Mrakibu Msaidizi (1986), Mrakibu wa Polisi(1991), Mrakibu Mwandamizi (1995), Kamishna Msaidizi wa Polisi (1998) na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (2002) hadi alipostaafu mwaka 2010.

 
Baadhi ya nafasi alizowahi kuzitumikia katika Jeshi la Polisi ni pamoja na kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) katika wilaya za Dodoma, Tarime, Serengeti na Arusha pamoja na Kuwa Mkuu wa Polisi wa Mkoa (RPC) katika mikoa ya Lindi, Arusha, Kigoma pamoja na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza ghasia Tanzania na hadi anastaafu alikuwa mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani Tanzania.

Thursday, October 10, 2013

KAZI PCCB




1.    Investigation Officers(214post)
Direct Entarants(From Colleges/Universities)
Applicants should posses thre yeas advanced diploma or undergraduate degree from recognized higher learning institutions in any of the following fields: Quantity Survey, Accountancy, Human Resources Management, Law, Procurement, Journalism, Information Technology, Highway Engineering, Building Constructions, Electrical Engineering,  Lamd management and Evaluation and Forensic Knowledge
Required Qualification:
-All applicants must be citizens of Tanzania not above 35 years old
-Applicants should have a minimum pass of lower second class
-Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
    -Degree/Advanced Diploma Transcript and certificates
    -Form four and form six National Examination certificates
    -Standard seven completion certificate
    -Professional certificates from respective boards(added advantage)
    -One recent passport size picture and birth certificate
    -Postgraduate Degree Transcripts and certicates(added advantage)
-Applicant should have good working knowledge of ICT(with related software,phone,fax,email,the internet and computer application eg MS Office)
-Applicants in th law field must have postgraduate diploma in legal practice(Law School oof Tanzania graduate) or passed the Bar exam and enrolled in the role of advocates.
Applicants in the Information Technology field must posses the following qualifications:
-Bachelor of science(BSc) in computer science/computer engineering/Electronics/Information Technology
-Certificate in A+ or Microsoft Certified Technology Specialist(MCTS) is an added advantage
-Data mining

2.0  Assistant Investigators(180 posts)
2.1 Personal Secretaries(8 Posts)
Qualifications:
-Applicants should posses Secondary School Certificates with passess in English and Kiswhili
-Diploma in Secretarial studies
-Short Hand 80 Wpm
-Computer literacy at least windows, microsoft office, internet,
e-mail, Microsoft publisher
Duties and Responsibilities:

-Performs Secretarial and Office management duties
-Keep custody of records, files, register and computer, e-mail, massages and ensure there  are properly channeled to respective destination
-Assist in coordinating secretarial function with other depatments
-Deal with all appointment Schedules for relevant officers
-Perform any other duties as may be assigned

2.2 Assistant Acountant(10 post)
Qualifications:
-Applicants should posses secondary school certificate with pass in english and kiswahili
-Applicants should also posses certicate in Accounting Technician 2(ATEC 2-NBAA) or Diploma in accountancy from recognized Institute
Duties and Responsibilities
-To issue cheque and prepare cheque book returns
-To prepare Unused Recipts Returns
-To maintain petty cash
-To prepare monthly statements or outstanding imprest
-To prepare imprest payment vouchers
-To prepare imprest journal vouchers
-To ensure all filing is done in timely and accurate manner


2.3 Watchmen(95 Posts)
Qualifications:
-Applicants should have completed form four or six and undergone voluntary Natinal Service Training
-Training in security guard duties,local military and fire fighting techniques is an added advantage
Duties and Responsibilities:
-To patrol arround the premises and buildings during the night according to the laid down procedure
-To secure security for buliding and other PCCB properties
-To check all gate passes at the main gate to ascertain that vehicles and other Properties,going out of the premises of the PCCB are authorized as shown in the gate pass and that the gate passes are authentic
-To check all visitors,vehicles and property coming into the premises of the PCCB through the main gate whether it is legitimate in relation to accompanying documentation
-To ensure that hazardous materials are not smuggled into premises
-To write a duty reports and Submit them to higher authorities
-To carry out any other tasks related to the above mentionedand functions of the PCCB that she/he may be assigned by the Head of Administration
-Any other duties that may be assigned by his/her superior

2.4 Drivers (25 Posts)
Qualification:
-Form four or six leavers with a class C driving Licence(more than three year driving experience)
-Applicants should also posses Certificate of Competence from the National Institute of Transport(NIT) Dar es salaam or Institute of Technology(DIT) or Vocatinal Education Training Authority(VETA)
Duties and Responsibilities:
-To manage and drive vehicles they are assigned in accordance with traffic regulations:
-To inspect the vehicle before and after a journey to ensure that it is in good condition
-To fill in the Log Books and ensure that the vehicle is used for authorized purpose only
-To advise the Bureau on repair and maintenance of the vehicle

2.5 Office Attendants (38 posts)
Qualifications:
-Applicants should have completed and passed form four or form six.
-Certificate or diploma in Record management,front office hospitality,customercare and other related fields is added advantage
Duties and Responsibilities:
-To clean the premises and buildings of the bureau
-Take massages and mail from one place to another within the premises or outside
-The office attendant is responsible to the office suprvisor and responsible fro taking proper custody of property of the bureau
-Swicth off all rights,air conditions,fans and any other electrical equipment that ought to cease operating after working hours

2.6 Technicians (4 Post)
Qualificatons:
-Possesion of a Secondary School Education Certificate
-Possesion of a FTC or Ordinary Diploma in a related field
Duties and Responsibilities:
-Undertake minor works repair and other facilities
-Conducting regular inspection of the working tolls and facilities
-Determining maintenance and repirs required(fax machine,photocopy,printers,electricity,air conditins,water and sewage system)
Basic attributes for above positions:
-Self Motivated
-Role Model
-Integrity and Profesional Ethics
-Strong Intepersonal Skills
Remuneration:
According to the government Circular
Mode of application:
-Interested candidates should send their applications enclosingtheir current CV's,copies of relevant academic certificates,having reliable physical address,posta address,email,telephone numbers,certified photocopies of birth certificate and recent passport size photograph
-Applicatants must submit three names of reliable referees
-Indicate in an envelope clearly a post you are applying for marked as "Application for the post of...."(insert post) and send your application letter to the following address:

The Director General,
Prevention and Combating of Corruption Bureau,
P.o.box 4865
Dar es salaam
Deadline of application:21st October,2013

"HAND DELIVERY IS NOT ACCEPTABLE"
Source:Dailynews 30th September,2013

Wednesday, October 9, 2013

LISHE BORA KWA WATOTO WADOGO




Kwa miezi sita ya kwanza katika maisha ya mtoto chakula pekee ambacho wataalamu wa afya wanashauri apewe ni maziwa ya mama tu. Kunyonyesha ndio njia ya kwanza kabisa kumpa mtoto chakula. Unapoanza kumpa mtoto vitu vingine kama maziwa ya kopo wakati ana miezi michache utoaji wako wa maziwa unaathirika maana jinsi mtoto anavyonyonya ndivyo jinsi maziwa yanavyotengenezwa ndio maana watu wengi wanavyoanza kazi na kumuacha mtoto nyumbani maziwa yao yanaanza kupungua. Faida za kunyonyesha maziwa ya mama ni pamoja na:

Maziwa ya mama yana virutubisho vingi vya asili ambavyo ni muhimu sana katika ukuaji na kinga kwa mtoto. Humlinda na magonjwa mengi ya utoto pamoja na ‘allergies’ mbalimbali.
·       Hukuwezesha kuwa na ukaribu na mtoto wako.
·       Hukupunguzia uwezekano wa kupata kansa ya matiti.
·       Ni bure na unaweza kumpatia maziwa wakati wowote bila usumbufu.

Wakati gani Uanze Vyakula Vingine

Mtoto wako akifikisha miezi 6 unaweza kuanza kumpatia vyakula vingine kidogo kidogo (Kuna ambao kutokana na sababu Fulani daktari huwashauri kuanza mtoto akiwa na miezi 4 hivyo ni  vyema ukiwasiliana na daktari wako kwanza). Mtoto akianza kupewa vyakula nje ya maziwa mapema kabla ya miezi 4 ni hatari kwa afya yake maana mfumo wake wa kusaga chakula unakuwa bado haujawa tayari. Unapoanza kumpa vyakula vingine hauachi kumnyonyesha, unyonyeshaji unaendelea hadi miaka miwili na nusu.

Dalili kuwa mtoto wako yupo tayari kuanza vyakula vingine ni:

·       Amefikisha miezi 6
·       Anaweza kushikilia kichwa juu ( shingo imekaza)
·       Anaweza kukaa kwa kuwekewa kitu ( mfano kiti chenye mkanda)
·       Unapompa chakula na kijiko anafungua mdomo kutaka kupokea au anageuza uso kwa kukataa
·       Akipokea chakula anakiweka mdomoni na kujaribu kumeza na sio kukisukuma nje na kuacha mdomo wazi.

Hakikisha mtoto wako yupo tayari kabla hujaanza kumpa chakula na usimlazimishe sana anapoanza maana anaweza kuchukia chakula, inawezekana hapendi chakula ulichompa jaribu kubadilisha uone anapenda nini. Kila mtoto ni tofauti na mwingine hivyo usimlinganishe mtoto wako na mwingine la muhimu ni kuhakikisha kuwa anauzito kulingana na umri wake na anaongezeka kwa kupanda chati.

Mnapokuwa mnakula mezani mtoto naye awe hapo ili kumpa hamu ya kula na sio kila wakati akila anakuwa peke yake. Mpe chakula akiwa na furaha na pia akiwa na njaa ili aweze kufurahia chakula chake. Kabla ya kubadilisha aina ya chakula mpe kwa siku 3-4 mfululizo ili aweze kukizoea na kama kitamletea madhara ujue hasa ni chakula gani. Usimchanganyie vyakula maana hutajua anapenda nini na kuchukia nini na pia kama kuna kitu kitamdhuru ukichanganya hautagundua kwa urahisi.
Miezi 6-9

Endelea kunyonyesha na anza kumpa vyakula vyenye madini ya chuma. Mtoto alishwe kwa ratiba inayoeleweka kila siku na katika ratiba hiyo hakikisha angalau mara moja kwa siku muda wake wa kula unakuwa sawa na muda wa familia yote ili muweze kula pamoja. Vyakula vyake viwe vimepondwapondwa kabisa ikiwezekana tumia blender na hakikisha anapata mlo kamili yani matunda, mbogamboga, mbegu, nafaka, nyama na samaki. Inashauriwa kutokuchanganya aina tofauti za nafaka kwenye unga mmoja unapomtengenezea uji, uwe na unga wa mahindi, ulezi,mchele n.k tofauti tofauti. Pika aina moja ya uji kwa wakati unaweza kufanya kwa wiki au vyovyote utakavyopenda.

Unapompa mboga au matunda anza na tunda moja moja kwa wakati. Osha vizuri matunda yako na katakata vizuri na kuponda ponda kisha mpe kiasi kidogo kwa wakati na kikibaki usikiweke, mtengenezee kile atakachokula tu. Matunda kama papai, parachichi na embe ni mazuri kwa kuanzia. Chemsha maharage, njegere au mboga za majani na kumpa supu kidogo kidogo, usiweke chumvi nyingi kidogo sana inatosha. Usimpe juisi za madukani, hakikisha unamtengenezea juisi wewe mwenyewe na usichanganye matunda mbalimbali kwenye juisi moja, na usiweke sukari kabisa.

Miezi 9-12

Katika umri huu mtoto anakuwa tayari amezoea ladha tofauti tofauti za vyakula mbalimbali nje ya maziwa. Anauwezo wa kukaa na kushikilia kitu kwa mikono yake na kuweka mdomoni hivyo anza kumpa matunda laini mkononi aanze kujifunza kula mwenyewe. Hakikisha vipande sio vidogo sana anavyoweza kumeza ili kuepuka hatari ya kukabwa. Kwa sababu pia atakuwa ameanza kuota meno atakuwa anapenda sana kutafuna tafuna. Katika umri huu pia unaweza kuanza kumpa kiini cha yai, ute wa yai hadi afike umri wa mwaka mmoja. Endelea kumnyonyesha ila kwa sasa anakula kwanza kisha ndio ananyonya maana akinyonya sana anaweza akakataa chakula. Usimpe chakula kimoja mfululizo kwa muda mrefu maana atakinai na kuanza kukataa chakula, mpe vyakula tofauti tofauti ili aendelee kupenda chakula.

Jinsi ya Kutengeneza Chakula cha Mtoto

Ni rahisi sana kutengeneza chakula cha mtoto nyumbani kwako. Osha mikono yako vizuri kabla ya kuandaa chakula na hakikisha unatumia vyombo visafi.

Matunda na mboga mboga: osha mboga zako vizuri kwa maji safi ( ya uvugu vugu) na kisha katakata na kubandika jikoni kwa chumvi kidogo sana bila mafuta. Ikichemka isage kwenye blender au ponda ponda iwe laini kabisa kisha mpe mtoto. Matunda osha pia kwa maji ya uvugu vugu, toa ganda la nje na kata vipande vikubwa kama unataka ale kwa mikono yake mwenyewe au ponda ponda na upe kwa kijiko.

Nyama na Samaki: Chemsha vipande vya nyama na maji kidogo na iive kwa moto wa kiasi hadi ilainike kabisa kisha isage kwenye mashine (food processor) na umpe na ile supu. Samaki vile vile ila samaki hakuna haja ya kuisaga maana ikiiva inalainika sana na ni rahisi kwa mtoto kula bila taabu (Kuwa makini sana na mifupa!).

Mbegu: Hapa nazungumzia maharage, kunde, choroko, njegere n.k Pika hadi ziive kabisa na kulainika kisha pondaponda na kumpa mtoto. Pia viazi na ndizi vinafaa sana kwa watoto, unaweza ukachanganya na supu ya samaki / nyama au na maziwa.

Nafaka: Usichanganye nafaka tofauti tofauti kwa ajili ya uji wa mtoto, inashauriwa kuwa na unga tofauti kwa kila nafaka. Unapopika uji unaweza kuweka karaga zilizosagwa ili kuongeza mafuta na vitamin kwenye lishe ya mtoto.

Usalama katika Kula
·       Hakikisha haumuachi mtoto mdogo na chakula au kinywaji bila uangalizi hata kama ni maziwa ya chupa asije akapaliwa. Usimpe mtoto chakula au maziwa akiwa amelala, analia au anacheka.
·       Usimpe chakula ambacho kinaweza kumkaba au kumpalia kama karanga, maindi, zabibu n.k
·       Kabla ya kumpa mtoto chakula hakikisha umekiangalia joto lake usije ukamuunguza mdomo.
·       Usafi wa mtayarishaji, mlishaji na mlishwaji ni muhimu san asana.