Magari ya moshi mawili yamegongana nchini Afrika Kusini karibu
na mji mkuu wa Pretoria. Takriban watu 100 walijeruhiwa.
Wauguzi walisema kwamba watu 20 walijeruhiwa vibaya katika ajali hiyo.
"Magari moshi yote mawili yalikuwa yamejaa wasafiri ambao husafiri kwenda
Pretoria kila siku , wakiwemo watoto wengi tu waliokuwa wanaelekea shuleni,"
Afrika Kusini inakarabati mtandao wake wa safari za gari moshi ambao
umezeeka.
Ajali hiyo ilitokea mapema asubuhi jana baada ya gari moshi mmoja lilipogongana na
lingine lililokuwa limeegeshwa karibu na Attridgeville, kamji kadogo magharibi
mwa Pretoria.