Meli hiyo ilikuwa na watu 460. Zaidi
ya miatatu hawajapatikana , wengine 164 wameokolewa na wengine wawili
wamethibitishwa kufariki.
Meli hiyo ikiwa kwenye muonekano wa kawaida
Meli hiyo ilipoanza kupinduka
Ikiwa imezama imebaki sehemu ya chini kabisa
Waokoaji wakiwa wamewasili eneo la ajali kwa ajili ya kuokoa abiria
Meli ya Korea Kusini iliyokuwa imewabeba zaidi ya
abiria mianne sitini ilizama kusini mwa pwani ya nchi hiyo Jumatano asubuh
Zaidi ya watu miatatu bado
hawajapatikana baada ya meli iliyokuwa imewabeba wanafunzi kuzama nchini Korea
Kusini.
Awali maafisa walikuwa wamesema kuwa
wengi wa abiria waliokuwa katika meli hiyo waliokolewa.
Baadhi ya walionusurika wamekuwa
wakielezea hali ilivyokuwa ya kutisha ndani ya meli ilipoanza kusimama kwa
kuyumba, ikiegemea upande mmoja na haraka kuanza kuzama.
"Kwa kweli kulikuwa na sauti
kubwa na meli ghafla ikaanza kuegemea upande mmoja," amesema abiria
aliyeokolewa, Kim Song-Muk.
"watu walikuwa wakihangaika
kukimbilia maeneo ya juu ya meli, lakini ilikuwa vigumu kufanya hivyo kutokana
na meli kupinduka."
Bado haijafahamika kilichosababisha
kuzama kwa meli hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa iliwabeba wanafunzi wa shule,
lakini watu walionusurika katika ajali hiyo wanatoa maelezo sawa kuhusu tukio
hilo la kutisha.
Kikosi cha Walinzi wa Pwani ya Korea
Kusini kimesema abiria wapatao mia tatu hawajulikani walipo baada ya meli
kupinduka na kuzama.
Watu wawili wamefahamika kupoteza
maisha na watu mia moja na sitini na wanne wameokolewa.
Wengi wa abiria wa meli hiyo
walikuwa wanafunzi wa sekondari wakiwa katika safari ya masomo kuelekea kisiwa
cha Jeju, nchini Korea Kusini.
0 Comment to "MELI YAZAMA KOREA KUSINI"
Post a Comment