Tuesday, April 15, 2014

UKRAINE NA RUSSIA WAENDELEZA MVUTANO




Waandamanaji wanaounga mkono Russia hapo Jumatau walikaidi tarehe ya mwisho ya serikali ya kuyaachia majengo walinashikilia  ili wapewe msamaha, huku  kaimu rais wa Ukraine akitishia  kutumia majeshi kuwadhibiti.

Dazeni ya waandamanaji walivunja madirisha kwenye makao makuu ya polisi huko mashariki mwa mji wa Horlivka  na kuwafunga pingu polisi wakati walipochukua udhibiti wa majengo hayo.

Rais wa Marekani Barack Obama alimwonya Rais wa Russia Vladmir Putin katika mazungumzo kwa njia ya simu  Jumatatu  kuwa Moscow itakabiliwa na gharama zaidi ikiwa hatua zake huko Ukraine zitaongezeka.

 Pia alimsihi kiongozi huyo wa Russia kutumia ushawishi wake kuwarai waandamanaji waondoke kwenye majengo wanayoshikilia.  Naye rais Putin alimsihi rais Obama kuiomba serikali ya Ukraine kutotumia nguvu dhidi ya waandamanaji.

Share this

0 Comment to "UKRAINE NA RUSSIA WAENDELEZA MVUTANO"

Post a Comment