Sunday, June 29, 2014

MSHAMBULIZI WA UHOLANZI ARJEN ROBBEN AMEKIRI KUJIANGUSHA




Mshambulizi wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa alidanganya timu yake ikapewa penalti ya ushindi lakini akasema alikuwa ametegwa.

Kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .

Herrera amesema kuwa Penalti hiyo dakika tatu kabla ya kukamilika kwa mechi hiyo haikufaa''hiyo ni njama ya FIFA kuiondoa Mexico kwenye kinyang'anyiro hicho.

Robben alianguka katika eneo la hatari la Mexico wakati Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1.

Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar

Share this

Artikel Terkait

0 Comment to "MSHAMBULIZI WA UHOLANZI ARJEN ROBBEN AMEKIRI KUJIANGUSHA"

Post a Comment