Thursday, September 18, 2014

WANANCHI WA SCOTLAND WAPIGA KULA YA MAONI

Wananchi wa Scotland wakiwa na mabango yao
Wananchi wakiwa kwenye foleni ya kupiga kula


Upigaji kura ya maoni nchini Scotland unaendelea  ambayo itaamua kama nchi hiyo inaondoka kwenye muungano wake wa miaka 307 na Uingereza na kuwa taifa huru.

Watu waliojitokeza katika kura ya maoni wamekua wengi kwa sababu zaidi ya watu milioni 4 na laki mbili walijiandikisha kupiga kura ambapo asilimia 97 ya watu hao wanastahili kufanya hivyo.

Wananchi wanapiga kura kwenye vituo 2,600 vya kupiga kura vilivyoko nchi nzima kwa kuchagua neno “Ndio” au “Hapana” kwenye swali la kura ya maoni linalouliza kwamba “Ni vyema Scotland iwe taifa huru?”.

Upande unaopinga kujitenga kwa umoja huo unasihi kwamba kura ya “Ndio” itaharibu uchumi wa Scotland na kuvuruga maisha ya kila mtu kama ushirika wa Uingereza ulioundwa mwaka 1707 unavunjika. 

Share this

Artikel Terkait

0 Comment to "WANANCHI WA SCOTLAND WAPIGA KULA YA MAONI"

Post a Comment