Chelsea imemaliza ziara yake barani Asia kwa kuifungwa timu ya mastaa wa
Indonesia ”Indonesia All-stars” mabao 8-1, lakini kikubwa zaidi
kwake ni jinsi wachezaji wake vijana walivyoonesha kiwango cha juu na morali ya
kufanya kazi naye.
Romelu Lukaku amedhihirisha utata wake wa kufumani nyavu baada ya kufunga
mabao manne na mchezaji aliyeko katika majaribio Chelsea ameonesha uwezo baada
ya kufunga bao leo katika dakika ya 50, hivyo kuendelea kujiwekea mazingira ya
kusajliliwa na Mourinho.
Kevin De Bruyne alicheza kwa kiwango cha juu wakiwa Bangkok na
Kuala Lumpur, pia Nathaniel Chalobah alionesha kiwango kikubwa
sana mjini Jakarta
Kikosi hicho cha Chelsea : Blackman (Schwarzer 46); Wallace
(Ivanovic 46), Cahill, Terry (Kalas 46), Bertrand (Cole 46); Chalobah (Essien
46), Van Ginkel (McEachran 60); Ramires (Feruz 60), Hazard (Piazon 60), Moses
(Traore 46); Ba (Lukaku 46).
Mabao yametiwa nyavuni na: Hazard (penalty) 21, Ramires 29, 56 Ba
32, Terry 45, Traore 50, Lukaku 52, 65.
Bao la Indonesia All-Stars limefungwa na Kalas (og) katika dakika
ya 67.
0 Comment to "CHELSEA YAIFUNGA INDONESIA ALL STARS 8-1"
Post a Comment