Sunday, June 29, 2014

MSHAMBULIZI WA UHOLANZI ARJEN ROBBEN AMEKIRI KUJIANGUSHA




Mshambulizi wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa alidanganya timu yake ikapewa penalti ya ushindi lakini akasema alikuwa ametegwa.

Kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .

Herrera amesema kuwa Penalti hiyo dakika tatu kabla ya kukamilika kwa mechi hiyo haikufaa''hiyo ni njama ya FIFA kuiondoa Mexico kwenye kinyang'anyiro hicho.

Robben alianguka katika eneo la hatari la Mexico wakati Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1.

Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar

Tuesday, June 17, 2014

MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO YATAJWA




Nafasi za kujiunga na kidato cha tano mwaka 2014  kwa wanafunzi waliomaliza mwaka jana zimetangazwa rasmi muda huu jijini dare s salaam na naibu waziri wa TAMISEMI  Bw KHASIM MAJALIWA  ambapo zaidi ya wanafunzi 16800 wamekosa nafasi hizo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo upungufu wa shule za kidato cha tano
      
Akitangaza majina na shule walizopangiwa wanafunzi hao Mh MAJALIWA amesema kuwa jumla ya wanafunzi 54085 sawa na alimilia 75.61 ya wanafunzi 71527 waliostahili kuingia kidato cha tano mwaka huu wamechaguliwa huku wavulanai ni 31352 wakati wasichana ni 22733 ambapo ni sawa na ongezeko la wanafunzi 20402 kwa kulinganisha na wanafunzi 33683 walochaguliwa mwaka jana.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule mbalimbali wataanza kuripot katika meneo yao tarehe 10 julai mwaka huu ambapo mwisho wa kufika katika shule walizopangiwa ni tarehe 30 julai mwaka huu ambapoamesema kuwa kwa wale ambao watakuwa hawajiripot hadi tarehe hiyo nafasi zao zitajazwa na waliokosa nafasi.

Monday, June 9, 2014

Tuesday, June 3, 2014

SCHOLARSHIPS FROM THE GOVERNMENT OF THE DEMOCRATIC PEOPLE’S REPUBLIC OF ALGERIA



SCHOLARSHIPS FROM THE GOVERNMENT OF THE DEMOCRATIC PEOPLE’S REPUBLIC OF ALGERIA TENABLE IN ACADEMIC YEAR 2014/2015

Applications are invited from qualified Tanzanians to pursue Undergraduate degree programs in Algeria for the year 2014/2015. The medium of instruction is French.

FIELDS OF STUDY
  • Medicine                
  • Economic, Management and Commercial Sciences.
  • Mathematics and Computer science
  • State Engineer in Telecommunications   
  • Science and Technology (Environmental Engineering)
  • Science and Technology (Architecture)
  • Science and Technology (Hydrocarbons and Chemistry)
  • Science and Technology ( Electronics)                      
  • Science of Earth and Universe (Hydrogeology) 
  • Science of Nature and Life  (Food Industry)
  • Science of Nature and Life (Biology and physiology of Organism)
  • Science of Nature and Life (Ecology and Environment)
  • Matter Sciences (Chemistry)
  • Matter Sciences (Physics)  
  • French Language
  
2. QUALIFICATIONS

      Applicants must:
  • Have completed and passed Advanced Certificate of Secondary Education and have obtained an average grade of ‘B’ in the relevant subjects.
  • not be admitted in Higher learning institutions
  • not be older than 25 years of age by September 2014
  • have good health

3. SELECTED CANDIDATES WILL;-
  • Not be allowed to change and be admitted to local Universities.
  • Have to purchase own ticket to Algeria and return ticket after completion of studies.
  • have to meet monthly Top Up Allowance
Needy students may apply for a loan from the Higher Education Students Loans Board to cover the above items.

4. MODE OF APPLICATION
  • All applicants must attach certified photocopies of Academic Certificates, Transcripts, and birth certificates
  • Applications from Zanzibar should be channeled through the Ministry of Education and Vocational Training, Zanzibar (Coordinating Office)
  • Applicants must indicate reliable contact telephone numbers.

  • All applications should be addressed to:
The Permanent Secretary
Ministry of Education and Vocational Training
P.O. Box 9121
DAR ES SALAAM  

so as to reach him not later than 15th June 2014.


Monday, June 2, 2014

PETER MUTHARIKA ASHINDA UCHAGUZI WA MALAWI

Peter Mutharika akisalimia wananchi



Rais Kikwete akisalimiana na Rais Joyce Banda aliyeondoka madarakani leo baada ya kushindwa uchaguzi na Peter Mutharika huku Kinana akionekana kwa mbali sana.


Kiongozi wa chama cha upinzani cha Democratic Progressive nchini Malawi, Peter Mutharika, ameapishwa leo kama rais wa nchi hiyo. Bw Mutharika mwenye umri wa miaka 74 alisema katika hotuba fupi kuwa kazi yake kubwa itakuwa kuwaunganisha wamalawi baada ya mvutano wa muda mrefu katika maswala ya uchaguzi.

Ametoa wito kwa washindani wake kuungana naye katika kujenga taifa. Maafisa uchaguzi Ijumaa walimtangaza Mutharika kama mshindi wa uchaguzi wa wiki iliyopita uliokuwa na utata na kumshinda rais aliyekuwa madarakani Joyce Banda.

Tume ya uchaguzi ya Malawi ilitangaza matokeo hayo Blantyre, saa kadha baada ya waandamanaji waliokuwa wakidai hesabu mpya ya kura kupambana na polisi katika mji wa Mangochi – kusini mwa nchi. Inaripotiwa kuwa mtu mmoja alifariki katika ghasia hizo.

Hesabu ya mwisho inayonyesha kuwa Bw Muthariki alipata kiasi cha asilimia 36 ya kura, na chama cha Malawi Congress cha Lazrous Chakwera kilipata asilimia 29. Rais Banda alimaliza na asilimia 20 tu ya kura. Bw Mutharika ni kaka wa rais wa zamani marehenu Bingu wa Mutharika.