Tuesday, September 10, 2013

UKRAINE VS. ENGLAND: DROO 0-0




England wametoka Sare ya 0-0 na Ukraine huko Kiev na kujikita kileleni mwa Kundi HENGLAND-LAMPARD_N_GERRARD la kuwania kufuzu kwenda Brazil Mwaka 2014 kwenye Fainali za Kombe la Dunia.

Zikiwa zimebaki Mechi mbili kwa kila Timu kwenye Kundi H, ambapo Mshindi wa Kundi pekee ndie anakwenda Brazil na Mshindi wa Pili anaangukia Mechi ya Mchujo, England wanaongoza Kundi kwa Pointi moja mbele ya Ukraine na Montenegro huku wakiwa na Mechi mbili za Nyumbani Uwanja wa Wembley zitakazochezwa Oktoba.

Mechi hizo za England ni dhidi ya Montenegro na Poland.

Katika Mechi nyingine ya Kundi H iliyochezwa leo, Poland wamewatwanga San Marino Bao 5-1.

NETHERLANDS na ITALY pia zimefanikiwa jana kuwa nchi za kwanza kutoka Barani Ulaya kufuzu kwenda kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwakani.
Timu ambazo tayari zipo fainali za kombe la dunia:
·       BRAZIL==WENYEJI
·       JAPAN
·       AUSTRALIA
·       IRAN
·       SOUTH KOREA
·       ITALY
·       NETHERLANDS

Share this

Artikel Terkait

0 Comment to "UKRAINE VS. ENGLAND: DROO 0-0"

Post a Comment