Mkuu wa Kikosi cha
Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga amewataka madereva wote nchini
kubadilisha leseni zao za zamani kwa kuwa zimebaki siku saba tu zoezi hilo
kumalizika, vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa.
Akizungumza jana jijini
Dar es Salaam, Mpinga alisema Machi 31, mwaka huu itakuwa mwisho wa madereva
wote kutumia leseni za zamani, na kwamba kwa waliokuwa bado hawajabadilisha
wafanye hima kubadilisha ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza.
“Machi 31 ndiyo mwisho
na hatutaongeza muda wa kubadilisha leseni, hivyo wananchi wakae wakijua,
nawaomba watumie wiki hii moja iliyobaki kubadilisha leseni zao,” alisema
Mpinga.
Alisema ifikapo Aprili
Mosi mwaka huu wanataka kuona kila dereva anakuwa na leseni mpya, kwani za
zamani hazitatambulika na kwamba atakayebainika na leseni ya zamani
atachukuliwa hatua za kisheria.
0 Comment to "LESENI MPYA MWISHO MARCH 31"
Post a Comment