Sunday, March 24, 2013

TAIFA STARS YAIADHIBU MOROCO 3 - 1

Ubao wa Matokeo unavyosomeka mara baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Timu ya Taifa ya Morocco
 
Kikosi cha kwanza cha Taifa Stars kilichocheza dhidi ya Morocco. Mpaka mwisho Taifa Stars 3 Morocco 1
 

Timu ya Taifa ya Soka ya Tanzania kwa upande wa wanaume, Taifa Stars, jana imewapa watanzania raha ya aina yake baada ya kuichabanga timu ya Morocco (Atlas Lions) kwa jumla ya magoli 3-1 katika mchezo wa kuwania tiketi ya kwenda kwenye fainali za Kombe La Dunia zitakazofanyikia nchini Brazil hapo mwakani. Ushindi huo wa kishindo umepatikana katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam.

Magoli ya Taifa Stars yaliwekwa kimiani na wachezaji Thomas Ulimwengu kunako dakika ya 46 ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Mwinyi Kazimoto. Magoli mengine yaliwekwa wavuni kupitia kwa Mbwana Samatta kunako dakika za 67 na 80 za mchezo. Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta wote ni wachezaji wa kulipwa wanaochezea timu ya TP Mazembe huko Congo DRC. Goli la kufutia machozi la Morocco lilifungwa na Youssef El-Arabi kunako dakika ya 94.

Kwa matokeo hayo, Taifa Stars hivi sasa inashika nafasi ya pili katika kundi (Kundi C) kwa kuwa na pointi 6 ikiwa ni pointi moja pungufu kutoka kwa Ivory Coast wanaoongoza kundi hilo. Morocco ni ya tatu ikiwa na pointi 2 wakati Gambia inashika mkia ikiwa na pointi 1


 
 

Share this

0 Comment to "TAIFA STARS YAIADHIBU MOROCO 3 - 1"

Post a Comment