Mkuu wa jeshi la Libya
amejiuzulu baada ya mapigano kati ya waandamanaji na wanamgambo wanaoiunga
mkono serikali kupelekea kufariki kwa
watu 31 katika mji wa mashariki wa Benghazi.
Ghasia zilizuka Jumamosi wakati waandamanaji mjini Benghazi walipovamia ngome ya kundi la
wanamgambo wa kiislam wanaolipwa na
serikali kusaidia kulinda usalama.
Waandamanaji hao
walikuwa wanadai wanamgambo waweke silaha chini na kujisalimisha kwa maafisa wa
majeshi ya Libya.
Mkuu wa majeshi ya
Libya Youssef al Mangush ambaye alikuwa msimamizi wa wanamgambo alijiuzulu Jumapili. Mkuu huyo amekosolewa kwa kuchelewa
kuunda jeshi la kitaifa na kuwaacha wanamgambo waongezeke.
0 Comment to "MKUU WA JESHI LA LIBYA AMEJIUZULU"
Post a Comment