Monday, May 27, 2013

RAIS OMAR AL BASHIR ANATISHIA KUFUNGA BOMBA LA MAFUTA



Rais wa Sudan Omar al Bashir anatishia kufunga bomba linalobeba mafuta kutoka Sudan Kusini kwenda kaskazini , anasema kusini inaunga mkono waasi.

Bw.Bashir alisema katika hotuba ya Televisheni Jumatatu kwamba Sudan itafunga bomba hilo  la mafuta, kama Sudan Kusini itawapa uungaji mkono wa aina yeyote waasi, katika  maeneo ya mpakani ya Kordofan Kusini na Blue Nile  na eneo lenye utete mkubwa la magharibi la Darfur.

Rais huyo akilindwa   na maafisa wa jeshi, alizungumza  baada ya jeshi kusema limechukua tena mji wa Abou Kershola kutoka kwa waasi huko Kordofan Kusini.

Share this

Artikel Terkait

0 Comment to "RAIS OMAR AL BASHIR ANATISHIA KUFUNGA BOMBA LA MAFUTA"

Post a Comment