Monday, February 25, 2013

MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA WA UCHAGUZI NCHINI KENYA ULIOFANYIKA JIONI YA JANA


Awali kulikuwa na taarifa kuwa mgombea wa Urais Uhuru Kenyatta alikuwa amesusia mdahalo huo akidai kuwa mdahalo wa kwanza waliokuwa wanauendesha mjadala wenyewe waliangazia sana swala la ICC na kuwafanya wagombea wengine kumlemea.

Uhuru pamoja na mgombea mwenza William Ruto, wanakabiliwa na kosa la kuwa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007/2008 katika mahakama ya ICC.

Duru zilisema kuwa Uhuru alisitisha kampeini zake leo ili kuweza kujiandaa vilivyo kwa mjadala huo.

Wagombea wengine akiwemo waziri mkuu Raila Odinga wanajiandaa kwa mjadala huo ambao jana jioni ulilipa kipao mbele swala la ardhi, sera za kigeni, na uchumi.

Kura za maoni zinaonyesha kuwa asilimia tisini ya wapiga kura wanaona mjadala huu una manufaa kwa wakenya. Asilimia themanini na tano walisema wako tayari kutazama mjadala huo.

Asilimia robaini ya wapiga kura waliohojiwa punde baada ya mjadala wa kwanza walisema wangempigia kura Uhuru Kenyatta wakati asilimia 33 walisema wangempigia kura Raila Odinga.Wawili hao ndio wagombea wakuu katika uchaguzi huu.

Share this

Artikel Terkait

0 Comment to "MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA WA UCHAGUZI NCHINI KENYA ULIOFANYIKA JIONI YA JANA"

Post a Comment