Maandamano nchini
Tunisia baada ya mauaji ya mwanasiasa wa upinzani Chokri Belaid
Waziri mkuu wa Tunisia
Hamadi Jebali, amejiuzulu baada ya kukosa kuafikia makubaliano kuhusu serikali
mpya.
Bwana Jebali,alikuwa
anajaribu kuunda serikali mpya kufuatia msukosuko wa kisiasa uliosababishwa na
mauaji ya mwanasiasa wa upinzani Chokri Belaid wiki mbili zilizopita.
Awali alisema alikuwa
tayari kujiuzulu ikiwa chama chake cha kiisilamu cha Ennahda hakingeunga mkono
mpango wake wa kuwateua wataalamu kama wanachama wa baraza la mawaziri.
Mauaji ya mwanasiasa
huyo yaliyofanyika Februari sita, yalisababisha maandamano na ghasia pamoja na
kujiuzulu kwa maafisa wa serikali.
''Niliapa kuwa ikiwa
mpango wangu haungefaulu, ningejiuzulu, na nimefanya hivyo,'' alisema bwana
Jebali baada ya kukutana na rais Moncef Marzouki.
Akitaja hatua yake kama
jambo la kusikitisha , alisema aliamua kujiuzulu ili kutimiza ahadi yake kwa
wananchi wa Tunisia.
"watu wetu wana
ndoto fulani, ambazo wanataka wanasiasa kuwatimizia. Laizima tuweze kuwaweka
imani watu wetu,'' alisisitiza Jebali.
Na aliongeza kuwa,
kukosa kufaulu kwa mpango wangu, haina maana kuwa Tunisia imefeli, au mapinduzi
hayakuwa na faida,'' akigusia mapinduzi ya kiraia yaliyofanyika miaka miwili
iliyopita ambapo rais wa zamani Zine al-Abidine Ben Ali alipinduliwa.
0 Comment to "WAZIRI MKUU WA TUNISIA AJIUZULU"
Post a Comment