Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vinavyoaminika, Bi Kidude amefariki
mjini Unguja baada ya kuugua kwa muda mfupi akiwa nyumbani kwake maeneo ya
Rahaleo.
Pia umri mkubwa nao unasemekana kuchangia kifo chake japo hadi mauti
yakimfika alikuwa hafahamu umri wake halisi.
Bi Kidude atakumbukwa sana kwa umahiri wake wa kuimba na kucheza licha
ya umri mkubwa aliokuwanao ambapo aliweza kutamba na nyimbo zake kadhaa kama Ya
Laiti, Muhogo wa Jang'ombe n.k.
Kutokana na umahiri wake, Bi Kidude aliweza kupata mialiko kadhaa ya
kutumbuiza katika nchi kadhaa za Ulaya ikiwamo Ujerumani.
Habari za uhakika zinasema kwamba mpaka mauti yakimfika Bi Kidude
alikuwa hajabahatika kupata mtoto.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.
0 Comment to "BI KIDUDE AFARIKI DUNIA"
Post a Comment