Hii ni baada ya Uhuru
kumshinda Raila Odinga katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe nne mwezi Machi
.
Wageni mashuhuri
wakiweno marais wa nchi kadhaa za Afrika pamoja na wanadiplomasia na maelfu ya
wananchi walishuhudia sherehe hizo katika uwanja wa michezo wa Kasarani
viungani mwa mji wa Nairobi.
Odinga hakuhudhuria
sherehe hizo baada ya jitihada zake kutaka mahakama ya juu zaidi kubatilisha
matokeo ya uchaguzi kukosa kufua dafu.
Kenyatta na naibu wake
William Ruto wanakabiliwa na kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama
ya uhalifu wa kivita ICC . Wanadaiwa kuwa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya
uchaguzi mkuu uliofanyika miaka mitano iliyopita.
Wakati huo wawili hao
walikuwa mahasimu wa kisiasa na wote wanakanusha madai dhidi yao.
Rais wa Sudan Omar
al-Bashir, ambaye mahakama ya ICC imetoa kibali cha kumkamata, kuhusiana na
vita katika jimbo la Darfur, hakufika nchini Kenya kwa sherehe hizo licha ya
kuwa alialikwa.
Kenyatta ni mwanawe
rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta, na amerithi mali nyingi sana .
Aidha Kenyatta ndiye
rais mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuongoza nchi. Ana umri wa miaka 51 na ni
mwanawe rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta.
Awali tulikuwa
tunakusimulia kwenye ukurasa huu yaliyokuwa yanajiri shereha za kuapishwa kwa
Uhuru ziliponoa nanga.
14:01 Rais wa Uganda
ambaye pia ni mwenyekiti wa jumuiya ya Afrika Mashariki, Yoweri Museveni
ahutubia wananchi na kumpongeza Kenyatta na naibu wake William Ruto, kwa
ushindi wao na hata akawasifu wakenya kwa kuendesha uchaguzi kwa njia ya amani
13:25 Kenyatta
akabidhiwa upanga na nakala ya katiba ya Kenya na rais mstaafu Mwai Kibaki
ishara kuwa amekuwa amiri mkuu wa majeshi ya Kenya
13:21 Uhuru Kenyatta
atawazwa rasmi kama rais wa Jamuhuri ya Kenya baada ya kukabidhiwa cheti
kilichotiwa saini naye Rais mpya mwenyewe
13:01 Vigelegele na
shangwe punde baada kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta kama rais wa nne wa Kenya
12:59 Uhuru Kenyatta
aapishwa kama rais mpya wa Kenya akiwa kando yake akiwa na mkewe Margaret
Kenyatta
12:58 Uhuru Kenyatta
ajiandaa kula kiapo chake
12:56 Jaji Mkuu wa
Kenya Willie Mutunga amtambulisha rais mteule wa Kenya kwa wakenya kuambatana
na sheria na matakwa ya katiba ya Kenya na kuchukua kiapo cha kushuhudia
kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta
12:23 Rais Mwai Kibaki
anayeondoka madarakani anakagua gwaride la heshima
12:03 Victor Otieno
kupitia Bofya facebook akiwa Nairobi anamshauri Uhuru kuwa amekosolewa na watu
wengi kuwa hawezi kuwatekelezea wakenya mahitaji yao. Sasa natoa changamoto
kwake kuwa afanye kazi na aweze kuwaonyesha kuwa maoni yao sio sawa na
ahakikishe kuwa katiba inatekelezwa kikamilifu.
11:45 Shangwe na
vigelegele akiwasili rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta
11:45 Waziri mkuu wa
Ethiopia Hailemariam Desalegn,pamoja na wageni wengine waheshimiwa wawasili
katika uwanja wa Kasarani akiwemo Rais mstaafu Daniel Moi.
11:35 Naibu rais mteule
William Ruto aliwasili na mkewe
0 Comment to "UHURU KENYATTA RAIS MPYA WA KENYA"
Post a Comment